Volker Renner
Mjumbe wa Bodi
Volker Renner ni mjumbe mashuhuri wa bodi ya FINCA Microfinance Bank Limited (“FINCA Tanzania”). Ana uzoefu wa zaidi ya miaka 20 ya uzoefu wa juu wa usimamizi na utawala katika huduma ndogo za fedha katika mabara manne. Kuanzia 2004 hadi 2016 alitumikia FINCA Impact Finance kama Makamu wa Rais wa Mikopo na Akiba, COO Kimataifa, na Mkurugenzi wa Kanda kwa kampuni tanzu za FINCA Eurasia. Kabla ya kujiunga na FINCA, Volker alishikilia nyadhifa kama Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya ProCredit (Ukraine), na alikuwa mshauri wa benki nchini Urusi na Ukraine. Volker amewahi kuwa mwenyekiti wa bodi, mjumbe wa bodi, na mjumbe/mwenyekiti masuala hatarishi ya kifedha, Ukaguzi, Rasilimali Watu na kamati zingine katika taasisi na benki nyingi ndogo za fedha. Kwa sasa ni mjumbe wa bodi katika taasisi saba za kifedha za mtandao wa FINCA Impact Finance zikiwemo Tanzania, Malawi, Georgia, Kosovo, Jordan, Afghanistan na Pakistan. Pia ni mjumbe wa bodi katika taasisi moja isiyo ya kifedha nchini Ujerumani.


