habari na matukio

Jifunze habari za hivi punde kuhusu FINCA Tanzania na kazi zetu katika jamii.

Maswali ya Vyombo vya Habari:  [email protected]

  • News 15-05-2025

    Katika kuadhimisha siku ya wanawake Duniani, Wanawake kutoka benki ya FINCA walipata wasaa wa kutembelea gereza la wanawake Segerea. Hii ilikuwa ni fursa ya kipekee kwa wanawake wa FINCA kuungana na kusaidia wanawake wenzao. Walipeleka mahitaji mbalimbali kwa wafungwa hawa wa gereza la Segerea. Mahitaji haya yalijumuisha vitu muhimu kama vile Sabuni, dippers za watoto, mafuta, nguo, na taulo za kike,n.k. Hii ikiwa ni msaada wa vitu kwa ajili ya matumizi mbalimbali katika maisha yao ya kila siku. Lengo la FINCA ni kuendelea kuigusa jamii na kuleta tabasamu kwa watu wenye changamoto na kuharakisha jitihada zao za kuboresha maisha yao. ...

  • News 15-05-2025

    Kama sehemu ya kuunga juhudi za kuisaidia jamii inayoihudumia, FINCA Tanzania mapema mwaka huu ilishiriki Mbio za Kimataifa za Kilimanjaro za mwaka 2025. Kwa ushiriki huo FINCA ilichangia kampeni ya “Tumaini la maisha” ambapo waandaaji wa mbio hizo walitoa 5% ya kila ada ya ushiriki kusaidia matibabu ya watoto wanaougua saratani. Washiriki kutoka FINCA walivalia mavazi yenye nembo ya “FINCA Runners” ambayo pia ilisaidia kwa nembo ya FINCA kuonekana kwa zaidi ya washirki 20,000 katika mbio hizo. Pongezi za dhati kwa Afisa Mkuu wa Biashara, Felician Girambo, ambaye alipata medali kwa kumaliza mbio za kilomita 21 kwa wakati.

  • News 19-06-2024

    Benki ya FINCA Tanzania inayo furaha kutangaza ufunguzi wa ofisi yake mpya huko Mafinga iliyoko karibu na soko la Mafinga. Mafinga ina idadi inayokua ya watu na muhimili wa kibiashara unaochipukia kwa kasi.